Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

COSOTA YAKABIDHIWA RASMI WIZARA YA HABARI

Posted on: July 15th, 2020

Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki (COSOTA) leo kimekabidhiwa rasmi kwa uongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara kilipokuwa awali.

Hafla ya makabidhiano ya Chama hicho imefanyika jijini Dar es Salaam baina ya Makatibu Wakuu wa Wizara hizo mbili na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa tasnia ya sanaa wakiwemo viongozi wa taasisi za Serikali, wasanii wa muziki, filamu, sanaa za maonesho na waandishi wa vitabu pamoja na miswada na wengineo.


Katika hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa tukio hilo ni matunda ya uamuzi makini wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli uliofanywa kwa wakati muafaka ambapo nchi yetu imeingia kwenye uchumi wa kipato cha kati.

“Tunamshukuru Rais Magufuli kwa kufanya uamuzi mgumu wenye manufaa kwa wasanii wa Tanzania kwa kuwa anatambua sanaa ina umuhimu mkubwa katika maisha ya binadamu hivyo wasanii wetu hawapaswi kuwa maskini,” alisema Dkt. Abbasi. 

Pia Dkt. Abbasi alieleza kuwa uamuzi wa kuihamisha COSOTA ulitekelezwa ndani ya saa 24 baada ya tamko la Rais Magufuli alilolitoa Julai 12 mwaka huu akiwa Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma na yeye kuahidi kuwa ataendelea na kanuni hiyo ya saa 24 za maajabu ya kiutendaji.

“Nawaahidi kuwa ndani ya saa 24 zijazo kuanzia muda huu mambo mawili yatatokea, kwanza nitakutana na Bodi ya COSOTA na kusikiliza mipango yao katika kutekeleza kivitendo COSOTA mpya yenye kupigania haki za wasanii, pili ndani ya saa 24 hizi nitakutana na menejimenti na wafanyakazi wote wa COSOTA kuona tena mikakati yao ya kumfanya msanii awe tajiri kwa kunufaika na kazi zake”, alieleza Dkt. Abbasi.

Aidha kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe alibainisha kuwa COSOTA ni taasisi muhimu katika kutunza na kulinda maslahi ya wasanii hivyo wizara yake itaendelea kutoa ushirikiano kwa chama hicho muda wowote itakapohitajika kwa ajili ya maendeleo ya wasanii na taifa kwa ujumla.

Naye Mtendaji Mkuu wa COSOTA, Bi. Doreen Sinare alieleza kuwa wanajivunia uongozi makini wa Rais. Dkt. John Pombe Magufuli kwani ndani ya miaka mitano ya uongozi wake chama hicho kimepata mafanikio makubwa ikiwemo kuanzishwa kwa Bodi ya COSOTA pamoja na kuhamishiwa kwenye wizara inayohusika na wadau wa sanaa.

“Tunaahidi kuendeleza mazuri yote tuliyotoka nayo Wizara ya Viwanda na tunatarajia Wizara ya Habari itatupatia ushirikiano zaidi ili kuendelea kusukuma gurudumu la maendeleo kwa wasanii wa Tanzania,” alisema Doreen.

Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki (COSOTA) kiliundwa mwaka 1999 kupitia Sheria namba 7 ya Hakimiliki na Hakishiriki (The Copyrights na Neighbouring Rights Act). 

 

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO