Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Majaliwa: Chaneli Mpya ya Utalii Kuvutia Watalii Wengi Nchini

Posted on: December 15th, 2018

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli mpya ya utalii inatarajiwa kuvutia watalii wengi zaidi kuja nchini sambamba na kuongeza pato la taifa.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam, alipokuwa akizindua chaneli hiyo ya utalii inayojulikana kama “Tanzania Safari channel” Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli hiyo mpya itatoa fursa ya kutangaza wanyama mbalimbali waliopo katika hifadhi za wanyama, utamaduni wa watanzania pamoja na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini ili kuvutia watu wengi zaidi kuja kufanya utalii na hatimaye kuongeza kiasi cha fedha kitachochangia katika pato la taifa.

“Chaneli hii ni njia muhimu ya kutangaza utalii ndani na nje ya nchi yetu, ambapo itaongeza idadi ya watu watakaotembelea Tanzania” alisema Waziri Mkuu Majaliwa

Waziri Mkuu Majaliwa aliongeza kuwa kwa sasa watalii wanaokuja nchini kwa mwaka ni milioni 1.3 , na matarajio ya Serikali ni kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia milioni 2 ifikapo mwaka 2020, hivyo chaneli hiyo ya utalii itasaidia katika kufikia lengo hilo la Serikali.

Naye, Waziri Utalii na Maliasili Dkt. Khamis Kigwangala alisema kuwa sekta ya utalii nchini inachangia asilimia 17.7 katika pato la taifa, na katika mwaka 2017 shilingi trilioni 5.04 zilipatikana kupitia sekta hiyo, na hivyo Serikali imeanza kutekeleza mikakati mbalimbali itakayo saidia kukuza utalii na kuongeza pato la taifa

Akitolea mfano  mikakati hiyo kuwa ni “kuimarisha masoko ambapo wataalamu wa utalii wameshafanya maonesho ya barabarani katika baadhi ya nchi na hivi karibuni watafanya maonesho hayo nchini China ili  kuongeza masoko mapya” alisema Waziri Kigwangala

Waziri huyo wa Maliasili na Utalii, alifafanua mikakati mingine ya wizara hiyo ni kuweka mabango yenye picha mbalimbali za vivutio vya utalii  katika barabara inayoelekea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Aidha, Waziri huyo ametoa fursa kwa wasanii mbalimbali wakiwemo wa filamu na  muziki kutumia sehemu za vivutio vya utalii nchini kwa ajili ya kutengeneza kazi zao za sanaa.

Kwa upande wake, mwakilishi wa Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale, kutoka Zanzibar,  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Habari, Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Saleh Yusuph Mnemo alisema kuwa chaneli hiyo inatarajiwa kuwasaidia watu wengi kufahamu vivutio vya utali vilivyopo nchini sambamba na kuongeza mapato, ambapo Zanzibar peke yake ina vivutio vya mambo ya kale 39.

Naibu Katibu Mkuu huyo, alifafanua kuwa asilimia 80 ya fedha za kigeni zinazopatikana Zanzibar zinatokana na sekta hiyo, huku ikichangia  asilimia 20 katika pato lake la taifa.

 Chaneli hiyo ya utalii inayojulikana kama Tanzania Safari Channel inaonekana kupitia kisimbuzi cha Startimes namba 331, na kurusha matangazo yake kwa lugha mbalimbali

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO