Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Serikali Yafafanuz Mawaziri Kuzungumza, Yaendelea Kueleza Utekeleza wa Ripoti ya CAG

Posted on: April 16th, 2018

TAARIFA KWA UMMA

Serikali Yafafanua Mawaziri Kuzungumza, Yaendelea Kueleza Utekelezaji Ripoti Ya Cag Sekta Za Kilimo Na Mifugo

Dodoma, April 16, 2018: 

Serikali imeendelea kueleza hatua za utekelezaji wa hoja za ukaguzi zilizoainishwa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2016/17 kwa kuainisha hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika Sekta za Kilimo na Mifugo huku ikifafanua misingi ya kikatiba na kisheria kwa mawaziri kujitokeza kufanya hivyo.

                          Dkt. Mwakyembe:Mawaziri Hawavunji Sheria    

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na waandishi wa habari Leo Mjini Dodoma na  kufafanua kuwa kitendo cha mawaziri kueleza utekeleza wa hoja za ukaguzi ni utamaduni mpya wa kiuwajibikaji unaoletwa na Serikali ya Awamu ya Tano

Kabla ya ufafanuzi kuhusu utekelezaji katika sekta za kilimo na mifugo, Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia kitaaluma ni mwanasheria aliyebobea katika masuala ya Katiba, amefafanua kuwa kitendo cha mawaziri kueleza utekelezaji wa hoja za ukaguzi ni utamaduni mpya wa kiuwajibikaji wa Serikali ya Awamu ya Tano na itachukua muda kuzoeleka lakini amewahakikishia Watanzania kuwa hakuna sheria yoyote ya nchi wala ya kimataifa iliyovunjwa.

Akieleza msingi wa kikatiba na kisheria wa hatua hiyo, Dkt. Mwakyembe aliitaja ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa pamoja na kutoa uhuru wa kupashana habari, Serikali inapewa wajibu wa kutoa taarifa kuhusu utekelezaji. Aliongeza zaidi kuwa misingi hiyo ya kikatiba imepambanuliwa zaidi katika Sheria ya Haki ya Kupata Taarifa na. 6 ya mwaka 2016.

“Hakuna sheria yoyote duniani sembuse hapa nchini inayoizuia Serikali kueleza utekelezaji ilioufanya katika jambo lolote lenye manufaa kwa umma. Kama yupo mwenye hicho kifungu kinachotuzuia mawaziri kueleza utekelezaji katika sekta zetu atuoneshe. Nashawishika tu kusema wanaoumizwa na hatua hii ni wale wasiotaka kusikia changamoto zinazowarudisha nyuma wananchi zikitatuliwa,” alisema.

Akiichambua Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya Mwaka 2008 (na mabadiliko ya mwaka 2013), Dkt. Mwakyembe alikitaja kifungu cha 38(1)-(3) kuwa zinaainisha hatua mbalimbali za kibunge kuhusu ripoti ya CAG pamoja na majibu ya Serikali yaliyoandaliwa na Maafisa Masuuli na kwa kuwa kuanzia hapo ripoti zote huwa wazi kwa umma si mawaziri tu bali hata wananchi wanaruhusiwa kuzisoma na kuzijadili.

                                    Dkt. Tizeba: CAG ametuonesha njia

Waziri wa  Kilimo, Dkt. Charles Tizeba  akiongea na waandishi wa habari Leo Mjini Dodoma ambapo alisema Kufuatia Taarifa ya CAG Wizara  imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kufanya ukaguzi wa kustukiza ili kubaini madawa feki lakini pia ilifika hatua wataalamu wa kilimo kutoka Wizarani na taasisi nyingine wapatao 200 wakapelekwa maeneo mbalimbali nchini kutoa elimu sahihi ya kukabiliana na visumbufu mimea.

 

Akizungumzia Sekta ya Kilimo, Dkt. Tizeba alisema sehemu kubwa ya ripoti ya CAG imegusa kwa usahihi changamoto mbalimbali katika udhibiti wa visumbufu vya mimea ambavyo hujumuisha pia wadudu wanaoshambulia mazao mbalimbali.

Alisema, tangu ukaguzi ulipobaini changamoto hizo Juni mwaka jana, Wizara imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kufanya ukaguzi wa kustukiza ili kubaini madawa feki lakini pia ilifika hatua wataalamu wa kilimo kutoka Wizarani na taasisi nyingine wapatao 200 wakapelekwa maeneo mbalimbali nchini kutoa elimu sahihi ya kukabiliana na visumbufu mimea.

Waziri Tizeba amesisitiza kuwa, mbali na hatua hizo, Wizara imeunda timu ya wataalamu kuchambua kila eneo lililobainishwa kuwa na mapungufu ili kuyatafutia ufumbuzi wa kudumu.

  •  
  • Waziri Mpina Avunja Bodi   
  • Kwa upande wake Waziri Mpina amesema kuwa CAG aliombwa kufanya ukaguzi maalum kuhusu ufanisi wa utendaji wa Kitengo cha Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (Tanzania Marine Parks And Reserves Unit) na ripoti yake imebaini udhaifu katika maeneo mengi.
  • “Taarifa ya ukaguzi wa ufanisi imebainisha udhaifu katika usimamizi wa maeneo ya hifadhi za bahari na maeneo tengefu. Hoja zilizobainishwa jumla ni 24 na zote zimebainisha changamoto kubwa kwa sababu ya udhaifu wa Menejimenti na Bodi ya Wadhamini,” alisema.
  • Kutokana na ukaguzi huo, Waziri Mpina alitangaza, kwa mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa Sheria ya Kitengo cha Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu na 29 ya mwaka 1994, amemsimamisha kazi Dkt. Milali Machumu, Meneja wa Kitengo hicho kupisha uchunguzi na ameivunja Bodi iliyokuwa chini ya Mwenyekiti Prof. John F. Machiwa ili kuiunda upya.
  • Katika mfululizo wa mawaziri kueleza utekelezaji, kesho itakuwa zamu ya Wizara za Afya na Elimu.

Imetolewa na:


Dkt. Hassan Abbasi,

Mkurugenzi, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO