Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Tanzania na Misri zaahidi kudumisha Ushirikiano na Mahusiano.

Posted on: August 15th, 2017

RAIS John Pombe Magufuli na Rais Abdel Fattah Al Sisi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri wameahidi kuongeza nguvu katika kuimarisha na kuendeleza uhusiano wa muda mrefu uliopo kati ya nchi zao.

Wakizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar Es Salaam mara baada ya kuongoza mkutano wa mashauriano kati ya Serikali za Tanzania na Misri, viongozi hao walisema kuwa katika mkutano huo pande mbili hizo zimekubaliana kuchukua hatua za haraka ili kuongeza kasi ya uhusiano na ushirikiano.

“Tumekubaliana kuongeza kasi ya uhusiano na ushirikiano wetu na katika kutekeleza hilo tumeamua kufufua Kamisheni ya Ushirikiano kati ya nchi zetu na kuagiza mikutano hiyo ya mashaurisno ifanyike kwa haraka”Rais Magufuli alieleza.

Alieleza kuwa Kamisheni hiyo ambayo ndio inayoratibu na kuongoza mashirikiano kati ya nchi hizo ilikutana kwa mara ya mwishio miaka 20 iliyopita hivyo kupunguza kasi ya mashirikiano katika baadhi ya maeneo.

Aliwaeleza waandishi wa habari kuwa Serikali hizo nimedhamiria kuimarisha uhusiano kati yao ikiwa ni sehemu ya kuienzi historia nzuri ya ushirikiano iliyoasisiwa na Rais Julius Nyerere na Gamal Abdel Nasser.

Katika mnasaba huo, nchi hizo zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika maeneo yanayoshirikiana sasa na kuangalia maeneo mengine zaidi kwa manufaa ya Serikali na wananchi wa pande zote mbili.

Rais Magufuli aliyataja mambo mengine waliyokubaliana kuwa ni pamoja na kupanua biashara na uwekezaji, kilimo, elimu, afya pamoja na ulinzi na usalama.

Alibanisha kuwa chini ya makubaliano hayo, Misri itaanzisha kiwanda kikubwa na kisasa cha nyama humu nchini ili nchi hiyo iweze kukidhi mahitaji yake ya nyama pamoja na kuuza katika masoko ya nje.

Halikadhalika, Misri imeahidi kupanua wigo wa misaada yake kwa Tanzania katika sekta za afya na elimu ambapo kwa upande wa afya nchi hiyo itaijengea uwezo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili iweze kufanya upasuaji wa figo ifikapo mwaka 2020.

Kwa upande wa elimu, Rais Magufuli alibainisha kuwa nchi hiyo imekubali kuongeza nafasi za masomo kwa vijana wa Tanzania ambapo alieleza kuwa kwa sasa watanzania 115 wako nchini humo wakichukua mafunzo katika fani mbali mbali.

 

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO