Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania

Posted on: September 11th, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 11 Septemba, 2017 amemuapisha Prof. Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

Prof. Ibrahim Hamis Juma anakuwa Jaji Mkuu wa nane baada ya uhuru na hafla ya kuapishwa kwake imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai.

Akizungumza baada ya kumuapisha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma na Majaji wengine wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani kwa kazi kubwa wanayofanya, na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa mhimili huo wa dola ikiwa ni pamoja kukabiliana na changamoto mbalimbali kulingana na uwezo wa kibajeti.

Mhe. Rais Magufuli ametoa wito kwa Jaji Mkuu, Majaji na Mahakimu wote wa mahakama nchini kuongeza kasi ya kufanyia kazi changamoto mbalimbali za mahakama ikiwemo ucheleweshaji wa kesi, na zaidi amewataka kuongeza msukumo katika kushughulikia tatizo la rushwa.

“Na ndio maana nimechukua muda mrefu kuteua Jaji Mkuu, kwanza nilitaka niteue Jaji Mkuu atakayekaa muda mrefu, sio baada ya miaka miwili nilazimike kuteua tena Jaji Mkuu, na pili nilitaka nijiridhishe huyu nitakayemteua ataweza kupambana na rushwa? Maana rushwa imetapakaa kila mahali, Serikalini kuna rushwa, Mahakamani kuna rushwa” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amesema hakumteua Prof. Ibrahim Hamis Juma kwa shinikizo la mtu yeyote na hivyo ametaka yeye pamoja na Majaji na Mahakimu wa mahakama nchini wafanye kazi kwa kutanguliza maslahi ya wananchi na Maslahi ya Taifa.

Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amemshukuru Jaji Mkuu Mstaafu Mhe. Mohamed Chande Othman kwa utumishi wake na ametoa wito kwa Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma kutosita kuwatumia Majaji Wakuu wastaafu ili kuendelea kupata uzoefu wao.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uteuzi huo na ameahidi kufanya kazi kwa mujibu wa Katiba huku akiwatoa hofu wananchi kuwa hakuna mgongano wowote katika mihimili ya dola hapa nchini, kwani kila mhimili una majukumu yake ya kuwasaidia wananchi.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO