Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Dkt. John Magufuli Awaapisha Mabalozi wa Tanzania Nchini Urusi na Rwanda

Posted on: March 21st, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 21 Machi, 2018 amewaapisha Meja Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi na IGP Mstaafu Ernest Jumbe Mangu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.

Hafla ya kuwaapisha Mabalozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza baada ya kuapishwa Mhe. Balozi Mumwi amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uteuzi huo na ameahidi kuwa katika kipindi chake atahakikisha uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi unaimarishwa na Tanzania inanufaika na uhusiano huo hususani katika azma yake ya kuvutia uwekezaji katika viwanda.

Kwa upande wake Mhe. Balozi Mangu pamoja na kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kumuamini ameahidi kuongeza msukumo katika utekelezaji wa ajenda muhimu za maendeleo kati ya Tanzania na Rwanda hususani ujenzi na manufaa ya mradi mkubwa wa reli ya kati utakaoiunganisha bandari ya Dar es Salaam na nchi nne za magharibi mwa Tanzania ikiwemo Rwanda. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Dkt. Susan Kolimba amewapongeza Mabalozi hao kwa kuteuliwa kuiwakilisha Tanzania nchini Urusi na Rwanda na ameahidi kuwa wizara hiyo itakuwa tayari wakati wote kutoa ushirikiano ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo diplomasia ya uchumi.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Mabalozi hao kufuatilia na kusimamia kwa ukaribu makubaliano mbalimbali ambayo Tanzania na nchi hizo wameyafikia ikiwemo miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Millicom International Services LLC inayomiliki kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Bw. Mauricio Ramos, Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo wamezungumza kuhusu uwekezaji wa kampuni hiyo hapa nchini.

Baada ya mazungumzo hayo Bw. Mauricio Ramos amesema amekuja kumweleza Mhe. Rais Magufuli kuhusu maendeleo ya kampuni hiyo ambayo imewekeza Dola za Marekani zaidi ya Bilioni 1 (sawa na zaidi ya Shilingi Trilioni 2.23 za Tanzania) katika miaka mitano iliyopita, imeajiri wafanyakazi zaidi ya 90,000 na kuwafikishia mawasiliano Watanzania kwa takribani asilimia 90.

Bw. Mauricio Ramos amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa jitihada zake za kupambana na rushwa na amebainisha kuwa juhudi hizo ni muhimu katika kuharakisha maendeleo na kupunguza umasikini.

Nae Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa Mnyaa amesema kampuni ya simu za mkononi ya Tigo ni ya pili kwa ukubwa hapa nchini ikiwa na wateja Milioni 11.06 na imekuwa ikilipa vizuri kodi ambapo mwaka 2017 ililipa kiasi cha Shilingi Bilioni 262.77.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli amekutana na watendaji wakuu wa kampuni ya Ferrostaal kutoka nchini Ujerumani na Denmark na Watendaji wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Nishati, ambapo wamejadili kuhusu mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha mbolea Mkoani Lindi.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage, Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani na Balozi wa Denmark hapa nchini Mhe. Einar Hebogard Jensen.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

21 Machi, 2018

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO