Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Dkt. Magufuli Apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi 5

Posted on: August 29th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Agosti, 2019 amepokea hati za utambulisho za Mabalozi 5 walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Mabalozi hao ni Mhe. Mahayub Buyema Mahafud (Balozi wa Jamhuri ya Saharawi hapa nchini), Mhe. Sanjiv Kohli (Balozi wa India hapa nchini), Mhe. Mej. Jen. Anselem Nhamo Sanyatwe (Balozi wa Jamhuri ya Zimbabwe hapa nchini), Mhe. Sandro Renato Agostinho De Oloveira (Balozi wa Jamhuri ya Angola hapa nchini) na Mhe. Mette Nørgaard Dissing Spandet (Balozi wa Denmark hapa nchini).

Katika mazungumzo, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza na kuwakaribisha Mabalozi hao hapa nchini Tanzania, na kuwahakikishia kuwa Tanzania inatambua uhusiano na ushirikiano mzuri na wa kihistoria na nchi zao na kwamba ipo tayari kuukuza na kuuimarisha zaidi uhusiano huo.

Mhe. Rais Magufuli amewataka Mabalozi hao kuungana na Tanzania katika juhudi kubwa za kuleta mageuzi ya kiuchumi na amewaomba wawaalike wafanyabiashara na wawekezaji wa nchi zao kuwekeza Tanzania halikadhalika wafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania kwenda kuwekeza katika nchi hizo.

Ametaja baadhi ya fursa zilizopo Tanzania kuwa ni ujenzi wa viwanda, ardhi kwa ajili ya kilimo na ufugaji, soko la uhakika na uwekezaji katika sekta ya gesi na mafuta.

Mabalozi hao wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kukaribishwa Tanzania na wameahidi kufanya juhudi kubwa za kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na nchi zao katika nyanja mbalimbali hasa uchumi na huduma za kijamii.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

29 Agosti, 2019

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO