Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Magufuli Aagiza Maafisa TANROADS Kusimamishwa Kazi

Posted on: March 16th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa aliyekuwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) katika Mkoa wa Morogoro Mhandisi Godwin Andalwisye na wahandisi wake 12 waliokuwa na jukumu la uangalizi wa barabara katika Mkoa huo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 16 Machi, 2020 baada ya kutembelea eneo la daraja la Kiegeya lililosombwa na maji ya mvua tarehe 02 Machi, 2020 na kusababisha kukatika kwa mawasiliano ya barabara ya Dodoma – Morogoro ambayo ni kiunganishi muhimu cha Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kaskazini Magharibi na nchi jirani za Uganda, Rwanda, Burundi na DRC ambazo husafirisha mizigo na abiria kwenda Dar es Salaam. 

Mawasiliano ya barabara hiyo yalirejea baada ya siku 2 na mpaka sasa eneo hilo linapitika kwa madaraja ya muda huku kazi ya kuimarisha ikiendelea.

Mhe. Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi kwa Maafisa hao wa TANROADS pamoja na kuwachunguza kama kuna vitendo vya hujuma walivifanya, kutokana na kutochukua tahadhari za kitaalamu za kuzuia maji ya mvua yasisombe daraja lililokuwepo na pia kushindwa kurejesha mawasiliano ya barabara kwa kujenga daraja haraka licha ya fedha za kufanyia kazi hizo kuwepo.

Katika mahojiano na Mkurugenzi wa Matengenezo wa TANROADS Mhandisi Mohamed Ntunda, Mhe. Rais Magufuli ameelezwa kuwa hadi daraja la Kiengeya linasombwa na maji ya mvua, TANROADS katika Mkoa wa Morogoro walikuwa na zaidi ya shilingi Bilioni 3 za matengenezo ya dharura ya barabara.

Akiwa katika eneo hilo Mhe. Rais Magufuli ameliona daraja la muda lililojengwa na Wataalamu wa TANROADS na pia ametembea kwa miguu kuelekea mto unakotirisha maji yake ambapo ameshauri wataalamu hao waangalie uwezekano wa kujenga daraja katika eneo jingine lenye umbali mfupi wa daraja na miinuko inayofaa endapo wataona inafaa kufanya hivyo.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuonya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Aloyce Kamwelwe, Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale na Mkurugenzi wa Matengenezo wa TANROADS Mhandisi Mohamed Ntunda kutokana na kutoridhishwa na juhudi zilizofanywa kurejesha mawasiliano ya uhakika katika eneo hilo na ametaka kosa hilo lisirudie.

Ametoa siku 7 kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na TANROADS kuhakikisha eneo hilo linakuwa na daraja la uhakika la kupita magari kama ilivyokuwa kabla ya daraja kusombwa na maji ili kutoathiri shughuli za kiuchumi na kijamii kutokana na kukatika kwa mawasiliano ya barabara.

Mhe. Rais Magufuli amewataka Mameneja wa TANROADS wa Mikoa yote hapa nchini kuhakikisha mawasiliano ya barabara kuu katika Mikoa yao hayakatiki vinginevyo meneja husika atavuliwa wadhifa wake.

Wasafiri na wananchi waliokusanyika katika eneo hilo wakati Mhe. Rais Magufuli akikagua eneo hilo wamelalamikia kukatika kwa mawasiliano ya barabara ya kuelekea Hospitali ya Misheni ya Berega kutokana na kusombwa kwa daraja, hivyo amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Loatha Sanare kuhakikisha Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inajenga daraja hilo ndani ya siku 7 ili wananchi waendelee kupata huduma za matibabu kama kawaida.

Halikadhalika wananchi hao wamelalamikia kutokamilika kwa ujenzi wa chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya Magubike na Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuhakikisha jengo hilo linajengwa ndani ya miezi 2.

Pia, Wananchi hao wamelalamikia kuchangishwa shilingi 20,000 kwa kila kaya kwa ajili ya kujenga jengo la maabara katika shule yao ya Sekondari, lakini fedha hizo hazijulikani zilikokwenda na badala yake wameanza kuchangishwa fedha nyingine shilingi 5,000 kwa kila kaya, na Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro Wilbroad Mutafungwa kufuatilia na kuchukua hatua stahiki. Mhe. Rais Magufuli amechangia shilingi Milioni 5 na ameagiza wananchi wasichangishwe fedha za ujenzi wa maabara hiyo.

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Morogoro

16 Machi, 2020

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO