Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Magufuli Ayataka Mataifa ya Afrika Kujiepusha na Masalia ya Fikra za Kikoloni

Posted on: August 29th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa Mataifa ya Afrika kutafsiri vizuri dhana ya uhuru na kujiepusha na masalia ya fikra za kikoloni za kuamini kuwa watawala wa zamani wa Mataifa ya Afrika ndio wenye uwezo wa kusaidia kusimamia na kuendeleza rasilimali zilipo katika Bara la Afrika.

Mhe. Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 29 Agosti, 2019 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipohutubia Mkutano wa 6 wa Jukwaa la Uongozi Afrika unaohudhuriwa na Marais Wastaafu Mhe. Benjamin William Mkapa (Tanzania), Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (Tanzania), Mhe. Thabo Mbeki (Afrika Kusini), Mhe. Hassan Mohamud (Somalia), Mhe. Hery Rajaonarimampianina (Madagascar), Mabalozi, Wawakilishi wa Kimataifa na washiriki wa Jukwaa la Uongozi Afrika.

Mhe. Rais Magufuli amefafanua kuwa dhana ya uhuru haiwezi kutenganishwa na kujitegemea kwani bila kujitegemea uhuru wa Taifa husika utakuwa mikononi mwa linayemtegemea.

“Maana hasa ya kupigania uhuru ilikuwa ni kurejesha rasilimali na hasa maliasili zetu lakini pia kuwa na maamuzi kamili kuhusu namna ya kuzisimamia na kuzitumia kwa manufaa yetu ili kuleta ukombozi wa kiuchumi, na hii ndio maana pekee ya kulinda uhuru wa kisiasa.

Tusijidanganye watawala wetu wa zamani hawawezi kugeuka kwa usiku mmoja na kuwa wajomba zetu au wakombozi wetu kiuchumi, utegemezi huu ndio umeimarisha mizizi na misingi ya ukoloni mamboleo, ni lazima tuamke” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Ametaja sababu ya 2 inayosababisha usimamizi mbaya wa rasilimali za Bara la Afrika kuwa ni tafsiri potofu ya msingi wa maendeleo kwa kudhani fedha ni msingi wa maendeleo hali iliyosababisha viongozi wake kuzunguka katika Mataifa tajiri kuomba misaada na mikopo ambayo inawezekana inatokana na rasilimali za Afrika, badala ya kuelekeza nguvu katika kusimamia na kutumia rasilimali zilizopo huku akisisitiza maneno ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyesema ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Sababu nyingine ni ukosefu wa ubunifu na teknolojia ya viwanda ambavyo vitaongeza thamani ya bidhaa za Afrika na kuzalisha ajira, migogoro na hali tete ya kisiasa inayosababishwa na mabeberu wanaotaka kuendelea kutumia maliasili za Afrika kwa manufaa yao, watendaji na viongozi wa Afrika kuingia mikataba mibovu na wawekezaji bila kujali maslahi ya Afrika kutokana na kukosekana kwa uzalendo na uharibifu wa maliasili unaosababishwa na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.

Mhe. Rais Magufuli amelipongeza Jukwaa la Uongozi Afrika kwa kuja na kauli mbiu isemayo “Kuimarisha Usimamizi Bora wa Maliasili kwa ajili ya Mageuzi ya Kijamii na Kiuchumi Afrika” na kubainisha kuwa kauli mbinu hiyo inaonesha umuhimu wa kujenga mifumo mipya ya kusimamia na kutumia rasilimali kwa manufaa ya watu wake.

Ametaja baadhi ya hatua zilizoanza kuchukuliwa na Tanzania katika kusimamia matumizi bora ya maliasili ili kufikia mageuzi ya kijani na kiuchumi kuwa ni kutunga sheria ya kulinda utajiri na rasilimali za Tanzania ya mwaka 2017, kupitia upya na kurekebisha mikataba ya uchimbaji wa madini isiyokuwa na manufaa kwa Taifa, kuweka msukumo mkubwa katika ujenzi wa viwanda na ukuzaji wa teknolojia ya viwanda na kudhibiti uharibifu wa maliasili za misitu na kulinda baionowai.

Hatua nyingine ni kutekeleza miradi mikubwa ya kuzalisha nishati ya umeme ukiwemo mradi mkubwa wa kujenga Bwawa la Nyerere katika mto Rufiji utakaozalisha megawati 2,115 za umeme, kuongeza maeneo ya uhifadhi kwa kuongeza Hifadhi za Taifa 3 mpya, kudhibiti nidhamu ya watumishi wa umma, kudhibiti ufisadi na ubadhirifu na kwamba matokeo ya hatua hizo yameanza kuonekana.

Washiriki wa mkutano huo unaofanyika kwa siku 2 wakiwemo Marais Wastaafu wameeleza umuhimu wa viongozi wa Afrika kutoa kipaumbele katika masuala muhimu yanayowahusu na kwa kushirikiana na kubadili mtazamo na fikra za utegemezi.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

29 Agosti, 2019

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO