Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Serikali ya Awamu ya Tano Yatekeleza kwa Kasi Hoja za CAG

Posted on: April 12th, 2018

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

IDARA YA HABARI-MAELEZO 

Dodoma, April 12, 2018: 

SIKU moja baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad kuwasilisha taarifa yake Bungeni na kisha kuongea na waandishi wa habari, Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha utendaji wa tofauti katika kutekeleza na kufanyiakazi hoja za ukaguzi.

Mawaziri wote ambao wizara zao zimeguswa na hoja mbalimbali za ukaguzi, pamoja na kuchukua hatua za haraka na kuwasilisha majibu rasmi Bungeni, kuanzia leo wataeleza kwa umma kupitia waandishi wa habari hatua walizozichukua za kufanyiakazi hoja husika.

Wakizungumza na waandishi wa habari leo mjini hapa, Dkt. Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, na Selemani Jafo, Waziri wa Nchi (Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), wakifungua mfululizo wa mikutano hiyo, wamesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, haitaruhusu fedha za umma zifanyiwe israfu.

Mawaziri hao wameipongeza Ofisi ya CAG kwa kazi nzuri kwani taarifa zake za ukaguzi zinasaidia lengo pana la Serikali ya Awamu ya Tano la kuhakikisha kila fedha inayokusudiwa kuwasaidia wananchi, inatumika ipasavyo ili kuyabadili maisha yao. 

                          Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali na hatua zinazochukuliwa na Serikali kutokana na ushauri uliotolewa katika ripoti hiyo, Wakati wa Mkutano Uliofanyika Leo Mjini Dodoma.


Dkt. Mpango: Tumerejesha Bilion 5 Zilizofujwa

Akijibu utekelezaji wa hoja ya kuwepo mafuta yaliyosamehewa kodi ya Shilingi bilioni 11.05 lakini yalitumiwa na makampuni yasiyostahili, Dkt. Mpango amesisitiza kuwa Serikali imefuatilia na kubaini hoja hiyo ni ya kweli. “Tayari Serikali imechukua hatua na kiasi cha Shilingi bilioni 5.53. Juhudi za kukusanya kiasi kilichobaki cha Shilingi bilioni 5.47 zinaendelea,” alisema.

Kuhusu hoja ya ongezeko la deni la matibabu nje ya nchi la shilingi bilioni 17.13, Waziri Mpango alisema deni hilo lilikua kutokana na wagonjwa wanaolazimika kusaidiwa matibabu ya muda mrefu nje ya nchi hasa saratani, kupandikizwa figo, mishipa ya fahamu, baadhi ya mahitaji ya upasuaji wa mifupa, moyo na baadhi ya magonjwa ya watoto.

Akifafanua hatua zilizochukuliwa kupunguza matumizi hayo miaka ijayo, Dkt. Mpango anasema kwa miaka ijayo mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tiba hizo zinapatikana hapa nchini na tayari mafanikio yamepatikana.

“Hospitali ya Muhimbili imeshaanza kupandikiza figo; hospitali ya Jakaya Kikwete inafanya upasuaji wa moyo; Hospitali ya Ocean Road inakamilisha kufunga mashine za kisasa, Hospitali ya Mloganzila ina vifaa vyote na tutaajiri wataalamu wa kutosha; Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma inakamilisha ufungaji vifaa vya kisasa, kuajiri mabigwa na imeshafanya upasuaji wa kwanza wa kupandikiza figo Machi, 2018,” alisema.

Kuhusu upungufu katika usimamizi wa fedha kwa mwaka 2016/2017, ambapo CAG amebaini ubadhirifu wa Shilingi milioni 332.86 katika Ubalozi wa Tanzania, Maputo, Msumbiji, Dkt. Mpango amesisitiza kuwa tayari mtumishi anayehusika amerejeshwa nyumbani na atafikishwa mahakamani. 


Waziri Jafo: Watumishi 434 Wamebanwa  

Akizungumzia hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika sekta zake, Waziri Jafo amewaeleza waandishi wa habari kuwa CAG kubaini vitabu 379 vya kukusanya mapato ndio havikuwasilishwa ni mafanikio kwani katika ukaguzi wa mwaka uliopita, idadi hiyo ilikuwa kubwa zaidi ikiwa ni vitabu 871. Alisema mfumo mpya wa kukusanya mapato kielektroniki utakomesha kabisa tatizo hilo.

Hata hivyo, Waziri Jafo amesisitiza kuwa kutokana na kasoro hiyo na nyingine za udhaifu na uzembe wa baadhi ya watendaji, Serikali haitafumbia macho hali hiyo. “Jumla ya watumishi 434 wamechukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu na kisheria baada ya kubainika kuwa wamezisababishia Halmashauri zao hasara au hoja za ukaguzi zisizo za lazima.” alisema.    

                                                                                        Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akieleza kwa waandishi wa habari leo mjini Dodoma kuhusu  hatua zilizochukuliwa na Serikali na zinazoendelea kuchukuliwa kutokana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali na hatua zinazochukuliwa na Serikali kutokana na ushauri uliotolewa katika ripoti hiyo akiwemo kuwafikisha watendaji waliofanya ubadhilifu wa fedha za umma kwa mujibu wa ripoti ya CAG.


Alizitaja hatua hizo na takwimu zake kuwa ni: watumishi tisa (9) wamefukuzwa kazi, watumishi 210 wamepewa barua za onyo, watumishi 15 wamefikishwa kwenye vyombo vya dola na watumishi 28 wamesimamishwa kazi.

Aidha, watumishi wengine 13 wametakiwa kufidia hasara walizozisababisha kutoka kwenye mishahara yao, watumishi wanne (4) wameshushwa vyeo, watumishi 10 wamebadilishwa majukumu, na watumishi 64 wapo katika mchakato wa hatua za kinidhamu.

Katika mfululizo wa mikutano hiyo kesho Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mhe. Charles Mwijage, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, watazungumza na waandishi wa habari saa 5:00 asubuhi kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Bungeni.

Imetolewa na:

 

Dkt. Hassan Abbasi,

Mkurugenzi, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO