Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Serikali ya Uingereza yaipatia Tanzania msaada wa Tsh. Trilioni 1

Posted on: August 24th, 2017

UINGEREZA imetoa msaada wa Dola za Marekani Milioni 450 sawa na takribani Shilingi Trilioni 1 za Tanzania kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Msaada huo umetangazwa Agosti 23, 2017 na Waziri wa Nchi anayeshughulikia maendeleo ya kimataifa na masuala ya Afrika katika Ofisi ya Mambo ya Nje na Jumuiya ya Madola ya Uingereza Mhe. Rory Stewart muda mfupi baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu Jijini Dar es Dar es Salaam.

Mhe. Rory Stewart amesema fedha hizo zitaelekezwa katika maeneo mbalimbali ya maendeleo hususani katika kuinua ubora wa elimu na kuongeza idadi ya watoto wanaopata elimu, kuimarisha miundombinu hasa barabara na bandari, kuinua kilimo cha kibiasharana viwanda kama vile viwanda vya pamba na nyama.

Mhe. Rory Stewart amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika mapambano dhidi ya rushwa na hatua zilizochukuliwa kuimarisha elimu kwa kuwapa nafasi Watanzania wengi zaidi kupata elimu.

“Nimetembelea shule moja hapa Dar es Salaam jana, na nimejionea jinsi sera ya kutoa elimu bila malipo ilivyoleta mabadiliko makubwa katika kuongeza idadi ya wanafunzi, nimezungukia shule, nimezungumza na wazazi na nimezungumza na walimu, idadi ya wanafunzi imeongezeka karibu mara mbili, hili ni jambo kubwa sana kutokea kwa muda mfupi na linaleta mabadiliko makubwa katika maisha ya watu, elimu ni kila kitu”amesema Mhe. Rory Stewart.

Amebainisha kuwa wananchi wa Uingereza wanaipenda Tanzania na Serikali yao itaendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ya uhusiano na ushirikiano na kwamba ana matumaini kuwa msaada ilioutoa utasaidia kuinua uchumi na maisha ya Watanzania.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Rory Stewart kwa kuja nchini na amemuomba ampelekee shukrani zake kwa Malkia Elizabeth II na Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe. Theresa May kwa msaada mkubwa uliotolewa kwa lengo na kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Mhe. Rais Magufuli amesema Uingereza ndio nchi inayoongoza kwa uwekezaji hapa nchini na amemhakikishia Mhe. Rory Stewart kuwa Tanzania inatambua mchango mkubwa wa nchini hiyo katika maendeleo ya Tanzania.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ametaka Watanzania waelewe kuwa hatua zinazochukuliwa na Serikali dhidi ya rushwa zina manufaa makubwa kwa nchi na amesema Serikali itahakikisha fedha za msaada zilitolewa na Uingereza zinasimamiwa vizuri.

“Na ndio maana tuwaomba Watanzania waendelee kutuunga mkono katika mapambano dhidi ya rushwa, rushwa ni ugonjwa mbaya sana, tukijisafisha katika rushwa nchi yetu itakwenda mbele, katika juhudi tunazofanya wapo wengine wanalalamikalalamika lakini matokeo yake ni makubwa na ndio maana ndugu zetu Waingereza wanaona.

“Pia nitoe wito kwa Watanzania kulipa kodi, hatuwezi siku zote tukawa tunategemea kodi za kutoka kwa nchi marafiki kama Uingereza, ni lazima tujenge mazingira ya Watanzania kuamini kuwa kulipa kodi ni kitu muhimu katika maendeleo yao” Amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Balozi wa Uingereza hapa nchini Mhe. Sarah Cooke, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO