Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Tanzania, Korea Zasaini Mkataba Ujenzi Daraja la Salander

Posted on: July 23rd, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Korea Mhe. Lee Nak-yon leo tarehe 23 Julai, 2018 wameshuhudia utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa daraja la Selander linalounganisha eneo la hospitali ya Agha Khan na Coco Beach kupitia baharini Jijini Dar es Salaam, litakalojengwa kwa muda wa miezi 36 kuanzia sasa.

Mkataba wa ujenzi huo umetiwa saini na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw. Jee Hoon Kim kwa niaba ya Kampuni ya ukandarasi ya GS Engineering and Construction ya Korea.

Daraja hilo pamoja na njia zake litakuwa na urefu wa kilometa 6.23, likiwemo daraja lenyewe lenye urefu wa kilometa 1.030, litakuwa na njia 4 na litagharimu zaidi ya shilingi Bilioni 250 za Tanzania hadi kukamilika kwake.

Akizungumza baada ya kutiwa saini kwa mkataba huo Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kutoa mkopo wa ujenzi wa daraja hilo, pamoja na miradi mingine ya maendeleo hapa nchini ikiwemo hospitali ya Taaluma na Tiba ya Mloganzila na daraja la Kikwete lililopo katika mto Malagarasi mkoani Kigoma, na ameahidi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendeleza na kukuza zaidi ushirikiano wake na Jamhuri ya Korea kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na wananchi wa Korea.

Mhe. Rais Magufuli ambaye kabla ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo amefanya mazungumzo na Mhe. Lee Nak-yon, amesema katika mazungumzo hayo ameiomba Korea kuendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mingine mikubwa ikiwemo utengenezaji wa meli kubwa katika ziwa Victoria ambayo mkataba wake utasainiwa hivi karibuni, ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (standard gauge) katika vipande vitatu vilivyobaki na ujenzi wa daraja kubwa la urefu wa kilometa 3.5 litakalounganisha eneo la Kigongo na Busisi katika ziwa Victoria.

Kwa upande wake Mhe. Lee Nak-yon amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa imani aliyonayo kwa nchi ya Korea na amemuahidi kwenda kufanyia kazi maombi ya kushiriki katika ujenzi wa reli ya kati na daraja la Busisi-Kigongo.

Mhe. Lee Nak-yon amemhakikishia Mhe. Rais Magufuli kuwa Korea ina kampuni zenye ujuzi mzuri, uzoefu na teknolojia bora katika ujenzi na utengenezaji wa meli na kwamba anaamini kuwa kupitia ushirikiano mzuri wa Tanzania na Korea, wataalamu wa Tanzania watanufaika na pia Korea itaendelea kutoa nafasi za masomo kwa Watanzania kwenda kujifunza utaalamu mbalimbali nchini humo.

Aidha, Mhe. Lee Nak-yon amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa juhudi zake za kupambana na rushwa, kujenga miundombinu, kuhimiza watu kuchapa kazi na kuboresha huduma za kijamii, na amebainisha kuwa mafanikio makubwa ambayo yameiwezesha Korea kutoka katika kundi la nchi masikini miaka 60 iliyopita, hadi kuwa nchi yenye pato la mtu linalofikia dola za Marekani 30,000 kwa mwaka hivi sasa yametokana na hatua kama zinazochukuliwa na Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Lee Nak-yon amemaliza ziara yake ya siku 3 hapa nchini na kuelekea nchini Oman.



Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

23 Julai, 2018

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO