Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Waziri Mkuu ameagiza Viwanda kutumia Barcodes za GSI

Posted on: February 22nd, 2018

Na Mwandishi Wetu-Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kila kiwanda kilichopo nchini kihakikishe kinatumia alama za utambuzi za GS1 Tanzania simbomilia (barcodes).

Ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Februari 22, 2018) wakati akifungua Mkutano wa Sita wa Wamiliki wa Viwanda na Watumiaji wa simbomilia (barcodes). Hadi sasa GS1 ina wanachama 2000.

“Natoa wito kwa wenye viwanda kutumia GS1 Tanzania kutangaza na kuuza bidhaa zenye ubora katika maduka ya kimataifa, ambapo pia bidhaa zao zitachangia katika ulipaji wa kodi kwa usahihi”.

Amesema matumizi ya alama hiyo, iwe ndio chanzo cha kulipeleka Taifa kwenye kampeni ya kuhamasisha jamii kununua bidhaa zilizotengenezwa nchini. Hadi sasa

Waziri Mkuu amesema kama kila bidhaa itakuwa na utambuzi wa Taifa kiambishi “620”, wataweza kuwa na takwimu sahihi za wazalishaji ambao wanatambulika.

Pia Waziri Mkuu amesema utambuzi wa bidhaa zinazozalishwa nchini ukifanyika kwa kutumia GS1 kila duka litalipa kodi kwa kila bidhaa inayouzwa.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema barcodes ni muhimu kwa sababu zinawawezesha wajasiriamali kuuza bidhaa zao katika maduka rasmi ya nje na ndani ya Tanzania.

Amesema miaka ya nyuma kabla ya kuanzishwa kwa GS1 Tanzania, wazalishaji wa bidhaa za Tanzania walilazimika kwenda nje ya nchi yetu kutafuta barcodes ili waweze kuuza bidhaa zao

Waziri Mkuu amesema hali hiyo iliifanya Tanzania kuwa wategemezi na kuchangia kuzalisha ajira kwa ajili ya nchi nyingine kwa kununua barcodes zao. “Tangu kuanzishwa kwa chombo chetu, tumejinasua kutoka katika utegemezi huo.

Pia Waziri Mkuu amesema amefurahishwa na mipango iliyowekwa na GS1 Tanzania ya kuhakikisha kwamba mazao ya kilimo yanapatiwa barcodes na kuwaelimisha wananchi kuhusu alama hizo.

Mkutano huo umehudhuriwa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara SMZ, Balozi Amina Salum Ally,  Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel.

Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania Dkt. Gidion Mazara, Wakuu wa Taasisi na Wadau wa GS1 kutoka Tanzania Bara na Visiwani (TBS, BRELA, TANTRADE, ZNCIAAL, COSTECH na Mtendaji Mkuu wa GS1 Tanzania Bi. Fatuma Kange.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

ALHAMISI, FEBRUARI 22, 2018.

Matangazo

  • Baraza la Mawaziri October 06, 2022
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Orodha ya Magazeti na Majarida ambayo Hayajahuisha Leseni ya Uchapishaji Serikalini February 05, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Mabadiliko Baraza la Mawaziri

    February 26, 2023
  • Uteuzi wa wakuu wapya wa Wilaya 37

    January 25, 2023
  • Mkutano wa Masuala ya Kilimo na Chakula Dakar nchini Senegal

    January 25, 2023
  • IMPORTANT NOTICE

    January 28, 2023
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2022 Habari MAELEZO