Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amaliza Mgogoro wa Ujenzi wa Makao Makuu ya Wilaya ya Mbinga

Posted on: January 6th, 2018

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemaliza mgogoro wa ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambao umedumu kwa miaka miwili.

Ametoa uamuzi huo jana jioni (Ijumaa, Januari 5, 2018) wakati akizungumza na watumishi na madiwani waHalmashauri ya Wilaya ya Mbinga pamoja na Halmashauri ya Mji wa Mbinga, kwenye ukumbi wa Jumba la Maendeleo, mjini Mbinga.

“Ninazo taarifa kuwa kuwa mnagombea mahali pa kujenga makao makuu ya Halmashauri hadi mnataka kujenga kwenye chanzo cha maji. Hiyo haikubaliki. Kwenye vyanzo vya maji hakujengwi miji, tena Afisa Maliasili nenda ukapande miti zaidi ili tutunze chanzo chetu,”alisema na kuamsha shange ukumbini. 

Wataalamu wa Halmashauri hiyowalikuwa wakivutana na Madiwani juu ya makao makuu hayo kujengwa Ndengu (ambako ni karibu na chanzo cha maji) huku wengine wakitaka yajengwe Kigonsera kwa madai kuwa kote ni karibu na wananchi.

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga iligawanywa Julai 2015 kwa kupata Halmashauri ya Mji wa Mbinga naHalmashauri ya Wilaya ya Mbinga na ilianza kazi Julai 2016. 

Waziri Mkuu alisema Halmashauri hiyo si ya kwanza kuwa na migogoro, kwa hiyo nimeamua mjenge hapahapa mjini Mbinga. Mkijenga huko wanakotaka hawa mtagombana na mkijenga kulenako pia mtagombana, lakini ugomvi wenu ni kwa faida ya nani? Kama si kuwaumiza wananchi mnaowaongoza ni nini?,” alihoji Waziri Mkuu. 

“Miaka yote mmekuwa mkipata huduma kutokea hapa hapa kabla Halmashauri hizi hazijatenganishwa. Tumeleta fedha mara mbili, mara ya kwanza sh. milioni 500 na ya pili sh. milioni 400 lakini hazijatumika kwa sababu ya migogoro yenu isiyo na tija. Kwa hiyo, makao makuu yatajengwa hapa hapa mjini,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu alisema kesi kama hizo zilishatokea Musoma Mjini na Vijijini, Lindi Mjini na Vijijini, Kigoma Mjini na Vijijini, na Singida Mjini na Vijijini ambako kote huko Halmashauri zaWilaya za Vijijini zimejengwa mjini na wananchi wanaendelea kupatiwa huduma kama kawaida. 

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amemuagiza Naibu Waziri (OR-TAMISEMI), Bw. Josephat Kakunda afuatilie sualala sh. milioni 700 ambazo zimetolewa na Serikali kwa ajili ya mradi wa majilakini Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imezitoa kwa kampuni ambayo haina hadhiya kupokea kiasi hicho cha fedha.

“Tumeleta kwa ajili ya mradiwa maji lakini ninyi mkaipa kazi kampuni ambayo haina hata uwezo wa kupokea sh.milioni 500. Ninazo taarifa kuwa Halmashauri hii mmeshalipa asilimia 80 ya fedha kwa mkandarasi huyo na wala maji hayajatoka hadi leo. Naibu Waziri fuatilia na nipate taarifa,”alisema.

 Waziri Mkuu anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma kwa kutembelea wilaya ya Nyasa ambako atazungumza na watumishi na madiwani, ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisiya Mkuu wa Wilaya, atakuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la utalii na pia kuhutubia mkutano wa hadhara.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO