Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Mageuzi ya Kisayansi Yazaa Matunda Sekta ya Madini

Posted on: May 30th, 2019

Na Mwandishi Wetu

Hatua za serikali kuhakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali za nchi yao na kuongeza mapato zimeanza kuzaa matunda licha ya kupingwa vikali hapo awali.

Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar-es-Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, amesema hatua zilizochukuliwa kwenye sekta ya madini  na kuboresha mifumo ya kukusanya mapato ya serikali imechangia kuongeza mapato maradufu.

          Akieleza hatua zilizochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano, Dkt. Abbasi amesema ni pamoja na ujenzi wa ukuta kwenye eneo la migodi ya madini ya Tanzanite Mirerani, kuanzishwa kwa masoko ya madini kwenye mikoa na wilaya nchi nzima na kuundwa kwa mifumo ya kisasa ya kijiditali ya kurekodi mapato ambayo licha ya kuongeza mapato, lakini pia imeongeza ufanisi.

          Dkt. Abbasi amesema kuwa hadi kufikia mwezi Mei 2019 sekta ya madini kwa kipindi cha miezi kumi na moja ya mwaka wa fedha 2018/19 mapato yamefikia Shilingi bilioni 302.63 kiasi ambacho ni zaidi ya mapato yote kiasi cha Shilingi bilioni 301.6 yaliyopatikana kwenye mwaka wa fedha 2017/18.

          Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Dkt. Abbasi mapato kwenye sekta ya madini katika kipindi cha miaka minne yamekuwa yakiongezeka mfululizo, akitolea mfano amesema mwaka 2016/17 makusanyo ya maduhuli yalikuwa bilioni 214.5 wakati mwaka 2015/16 maduhuli yalikuwa Shilingi Bilioni 210 na mapatao ya mwaka 2017/18 yalikuwa Shilingi bilioni 301.6

          Aidha, aliongeza kuwa mapato yanayotokana na mauzo ya madini ya Tanzanite tangu ujenzi wa ukuta wa Mirerani ujengwe kuzunguka migodi ya madini hayo mapato yameongezeka maradufu kutoka kiasi cha shilingi milioni 71.8 mwaka 2015 hadi kufikia bilioni 1.43 mwaka 2017.

Akieleza mafanikio yaliyopatikana kutokana na uboreshaji wa mifumo ya kukusanya mapato Dkt. Abbasi amesema mifumo hiyo sio tu imeongeza mapato, lakini pia imeongeza ufanisi.

“Kabla ya Mfumo wa TTMS Serikali ilikuwa haipati kitu kabisa katika miito ya simu za nje wala kuwa na uwezo wa kuhakiki mapato ya simu za ndani lakini tangu mfumo huo ulipofungwa kwa eneo la mapato ya simu za nje tu Serikali imekwisha kusanya Shilingi bilioni 97.16 ikiwa ni malipo ya kodi zitokanazo na mapato ya kampuni za simu kwa simu kimataifa zinazoingia na kuishia hapa nchini” alifafanua Dkt. Abbasi.

Kuhusu ziara ya Rais Magufuli kwenye nchi za Afrika Kusini, Namibia na Zimbabwe Dkt. Abbasi ameeleza ziara hiyo licha ya kuwa na lengo la kuimarisha ushirikiano wa kihistoria, lakini pia ilikuwa na lengo la kutafuta fursa za kibiashara. “Kwenye ziara hiyo Rais Magufuli ameweza kufikia makubaliano ya kuongeza kiwango cha biashara na uwekezaji kwenye sekta ya utalii, usafiri wa anga na miundombinu pia Tanzania imeweza kupata soko la mahindi tani 700,000 nchini Zimbabwe”.

Aidha, Dkt. Abbasi amewasihi Watanzania wenye ujuzi wa kufundisha Lugha ya Kiswahili kuitumia vyema fursa ya kufundisha lugha hiyo nchini Afrika Kusini kwa kujisajili kwenye kanzi data ya wataalamu wa Kiswahili Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) ili wapate ithibati na kutambulika rasmi.

          Kuhusu ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, Msemaji Mkuu wa Serikali amewahakikishia Watanzania majadiliano juu ya mrad huo bado yanaendelea na Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha maslahi ya nchi yanawekwa mbele ili wanufaike na rasilimali za nchi yao.

          Mkutano wa Msemaji Mkuu wa Serikali na vyombo vya habari umelenga kueleza  utekelezaji wa serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo madini, miundombinu, mawsiliano na sekta nyingine.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO