Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Dkt. Magufuli Aitangaza Dodoma Kuwa Jiji

Posted on: April 26th, 2018

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza rasmi kwa mamlaka aliyonayo kuipandisha hadhi Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji.

Dkt. Magufuli ameyasema hayo leo Mkoani Dodoma wakati wa Maadhimisho ya Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyoadhimishwa Uwanja wa Jamhuri mkoani humo.

“Tuliona Dar es Salaam ilivyokuwa makao makuu kipindi hicho na ilikuwa inaitwa Jiji, nikaona niangalie katika nchi yetu kuna Majiji mangapi, tuna Manispaa ngapi, Halmashauri ngapi na mimi nina mamlaka gani katika kutengeneza Majiji au Manispaa, nikakuta Dar es Salaam ni Jiji, Tanga ni Jiji, Arusha ni Jiji, Mwanza ni Jiji, Mbeya ni Jiji nikaambiwa Dodoma ni Manispaa nikasema hili haliwezekani kwa hiyo kuanzia leo kwa mamlaka waliyonipa Watanzania Dodoma ni Jiji”

“Kwa hiyo maandalizi yote ya kisheria lazima yaanze sasa kufanyika na huyu Mkurugenzi aliyekuwa wa Manispaa hapa hapa leo anakuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na hili litakuwa Jiji la peke yake kwa sababu lipo katikati ya Tanzania” ameongeza Dkt. Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli amesema kuwa anatarajia kufanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Dkt. Akinwumi Ayodeji Adesina ambao wanafadhili miradi 25 hapa nchini yenye thamani ya Dola Bilioni 1.986, ili kati ya miradi mbalimbali atakayoongea, Dodoma ipewa kipaumbele kama Jiji.

Akizungumzia kuhusu miaka 54 ya Muungano Rais Magufuli amesema kuwa, Tanzania imekuwa na mafanikio mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa maeneo ya ushirikiano, ambapo mwaka 1964 yalikuwa maeneo 11 na sasa yapo maeneo 22, Muungano umefanya  nchi imekuwa na sauti na kujiamini, vile vile kutoa mchango katika masuala mbalimbali ya Kimataifa na kusuluhisha migogoro.

Mbali na hayo Rais Magufuli amewataka Wananchi kulinda na kuudumisha Muungano uliopo na kutoa ushiririkiano kwa vyombo vya usalama kwani Muungano huo ni tunu kwa Taifa.

“Kikubwa kwa Watanzania bila kujali dini, kabila, vyama tusimame imara, tutunze na kuusimamia huu Muungano kwa nguvu zetu zote, Serikali ninayoiongoza na Serikali ya Zanzibar tupo imara, Muungano huu tutaulinda kwa nguvu zote, tutautunza na kuusimamia” amesisitiza Dkt. Magufuli.

Tanzania imeadhimisha Sherehe za miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibari ambapo Maadhimisho hayo yamebeba kauli mbiu isemayo “Muungano wetu ni wa mfano Duniani tuuenzi, tuulinde, tuuimarishe na kuudumisha kwa maendeleo ya Taifa letu”

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO