Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Dkt. Magufuli alipowajulia hali Majeruhi wa ajali ya Moto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Posted on: August 11th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewatembelea na kuwapa pole majeruhi waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam ambao wameungua moto katika ajali iliyotokea jana asubuhi Mjini Morogoro baada ya mafuta yaliyokuwa yakimwagika kutoka kwenye lori lililopinduka kulipuka moto. Ajali hiyo imesababisha vifo vya watu 71 mpaka sasa.

Majeruhi 46 wamefikishwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbi kwa magari ya wagonjwa na helkopta na majeruhi wengine wanaendelea kupatiwa matibabu Mkoani Morogoro.

Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Lawrence Museru na Mkuu wa Kitengo cha Wagonjwa wa Dharura cha hospitali hiyo Dkt. Juma Mfinanga wamemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa wagonjwa 46 waliofikishwa hospitalini hapo ni wale walioungua kwa kiwango kikubwa cha hadi takribani asilimia 100 na kwamba 3 kati yao wamefariki dunia baada ya kufika.

Pamoja na kuwapa pole, Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania kutokuwa wepesi wa kuwahukumu kwa madai walikuwa wakiiba mafuta, kwani baadhi yao walikwenda eneo la tukio kwa lengo la kutoa msaada, wengine walikutwa na moto wakiwa katika maeneo yao ya kazi na wengine walikutwa na moto wakiwa wanasafiri katika magari yao.

Mhe. Rais Magufuli amewashukuru Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Hospitali ya Taifa Muhimbili na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa juhudi kubwa wanazozifanya kutoa matibabu kwa majeruhi hao na ameagiza kuwa gharama za matibabu na huduma nyingine kwa majeruhi hao zitatolewa na Serikali.

“Nawashukuru sana Madaktari na Manesi, wanafanya kazi kubwa sana, kweli wanafanya kazi kubwa sana, nimewaona wagonjwa wanahudumiwa vizuri, lakini kikubwa sisi Watanzania tumtangulize Mungu mbele, tuwaombee hawa wagonjwa, lakini na wale waliotangulia mbele za haki nao tuwaombee, na niwaombe ndugu zangu Watanzania katika ajali tusiwe wepesi wa kuhukumu, nimefika humu wodini nimemkuta mmoja ni dereva wa lori la mafuta, alipofika pale aliamua kushuka aende akasaidie, lakini nae ameungua na amelazwa hapa, yupo mwingine alikuwa anasafiri kwenda Mtwara, wala hakwenda kuchukua mafuta, nae ameungua” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli alipokuwa akizungumza na wananchi waliokuwa nje ya wodi ya Kibasila.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuwatangaza majeruhi wote kwa majina yao na mahali wanakotoka ili ndugu na jamaa zao wapate taarifa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Lawrence Museru kumruhusu Bi. Rahel Kitwai Roita mkazi wa Turiani Morogoro kuuchukua mwili wa Marehemu mama yake, baada ya mwili huo kuzuiwa kutokana na kudaiwa zaidi ya shilingi Milioni 5 ambazo ni gharama za matibabu.

Bi. Rahel Kitwai Roita ametoa ombi hilo akiwa pembezoni mwa njia ya kupita wagonjwa ambapo Mhe. Rais Magufuli ametaka deni hilo la shilingi Milioni 5 adaiwe yeye na ametoa rambirambi ya shilingi laki 5.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

11 Agosti, 2019

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO