• Wasiliana Nasi
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Baruapepe za Watumishi
    • Malalamiko
TANZANIA INFORMATION SERVICES-MAELEZO
TANZANIA INFORMATION SERVICES-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo IDARA YA HABARI-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Magufuli azindua Kitabu cha Maisha binafsi ya Rais Msaafu Benjamin Mkapa

Posted on: November 12th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 12 Novemba, 2019 amezindua kitabu cha maisha binafsi ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa kiitwacho “My Life, My Purpose” (Maisha Yangu, Kusudio Langu).

Sherehe za uzinduzi wa kitabu hicho zimefanyika katika ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe. Dkt. Ali Hassan Mwinyi na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Wengine ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Mawaziri Wakuu Wastaafu, Mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Majaji Wakuu Wastaafu, viongozi wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mabalozi, Wabunge, viongozi wastaafu waliofanya kazi na Mhe. Mkapa akiwa Rais, viongozi wa Taasisi mbalimbali na Wakuu wa Mikoa.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Mstaafu Mkapa kwa kuandika kitabu kuhusu maisha yake kuanzia alipozaliwa mwaka 1938 katika Kijiji cha Lupaso, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, safari yake ya masomo, siasa na uongozi alipokuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya mwaka 1995 na mwaka 2005, kwa kuwa kitabu hicho kitawasadia Watanzania na watu wengine duniani kujifunza na kufahamu mchango mkubwa alioutoa kwa Taifa la Tanzania na katika Jumuiya ya kimataifa katika masuala ya maendeleo na uongozi.

Mhe. Rais Magufuli amekiri kuwa Mhe. Rais Mstaafu Mkapa ni mfano wake wa kuigwa na amemshukuru kwa mchango wake mkubwa katika safari yake ya siasa na uongozi kuanzia mwaka 1995 alipomnadi katika kampeni za Uchaguzi Mkuu akigombea Ubunge, alipomteua kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na baadaye Waziri wa Ujenzi, alipokubali ushauri wake akiwa katika nyadhifa hizo na alipomtia moyo katika uamuzi wake wa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015.

Ametaja moja ya ushauri ulioungwa mkono na Mhe. Rais Mstaafu Mkapa kuwa ni Serikali ya Tanzania kuanza kujenga barabara za lami kwa kutumia fedha za ndani kwa kutenga shilingi Bilioni 1.85 kila mwezi, na kusimamia kwa karibu utendaji wa Wizara hali iliyopelekea aitwe jina la utani la Askari wa Mwamvuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Mstaafu Mkapa kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania na kupiga vita umasikini kwa kuanzisha mikakati mbalimbali ikiwemo Mkakati wa Kukuza na Kuondoa Umasikini Tanzania (MKUKUTA), Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM).

Mhe. Rais Magufuli ameelezea kufurahishwa na juhudi zilizofanywa na Mhe. Rais Mkapa katika kukuza uchumi, kuondokana na utegemezi na kudumisha amani, na kwamba ni kutokana na hilo hata Serikali ya Awamu ya Tano anayoiongoza inasimamia mwelekeo huo.

Pamoja na kuipongeza Taasisi ya Uongozi kwa kuandika kumbukumbu za viongozi, ameitaka taasisi hiyo kuchapisha kitabu cha maisha binafsi ya Mhe. Rais Mstaafu Mkapa kwa lugha ya Kiswahili ili Watanzania wengi waweze kusoma, na ametoa wito kwa viongozi wengine wakiwemo wa ngazi za chini kuandika vitabu kuhusu maisha yao.

Kwa upande wake Mhe. Rais Mstaafu Mkapa, amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kukubali kuzindua kitabu chake na amempongeza kwa msimamo wake wa kuhakikisha Tanzania inajitegemea hasa katika maendeleo.

Mhe. Rais Mstaafu Mkapa amewashukuru wote walioshiriki katika uandaaji na uchapishaji wa kitabu cha maisha yake binafsi na amesema pamoja na kuandika kuhusu maisha yake, katika kitabu hicho ameeleza jinsi alivyofanya kazi na kumfahamu Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambaye fikra zake bado zipo hai na zina mashiko mpaka sasa.

Uzinduzi wa kitabu cha maisha binafsi ya Rais Mstaafu Mkapa, umekwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 81 ya tangu kuzaliwa kwake, ambapo viongozi waliohudhuria sherehe hizo wamepata nafasi ya kumpongeza, kumtakia afya njema na maisha marefu na pia wameshiriki nae chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa heshima yake na Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

12 Novemba, 2019

Matangazo

  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Orodha ya Magazeti na Majarida ambayo Hayajahuisha Leseni ya Uchapishaji Serikalini February 05, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais Magufuli atunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa

    November 21, 2019
  • Rais Magufuli azindua Kitabu cha Maisha binafsi ya Rais Msaafu Benjamin Mkapa

    November 12, 2019
  • Rais Magufuli akutana na viongozi wa AALCO

    October 24, 2019
  • Afrika ni muhimu kwa Maendeleo ya Uchumi wa Dunia- Putin

    October 24, 2019
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: 25 Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@habari.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka 2017/18
  • Tamko la Serikali kuhusu Matumizi ya Picha za Marais Wastaafu katika Sakata la Usafirishaji wa Mchanga wa Madini
  • Hotuba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe akifungua mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Mitaa Tanzania (ALAT)
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2019 GWF. Haki zote zimehifadhiwa.