Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Rais Magufuli Ang'ara Afrika Kiuchumi, Utawala Bora

Posted on: February 5th, 2019

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kung’ara kimataifa katika mapambano dhidi ya rushwa na utawala bora.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi leo Jijini Dodoma, wakati akiongea na Waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa masuala mbalimbali ya Serikali.

“Kutokana na utendaji wa kimageuzi wa Rais Magufuli, licha ya juhudi za watu wachache kuhaha kutaka kuichafua nchi yetu kimataifa, Tanzania imeendelea kuwa na taswira nzuri na heshima kubwa na ikiendelea kukubalika sana miongoni mwa Mataifa mbalimbali” amesema Dkt. Abbas

Dkt. Abbasi amefafanua kuwa, kimataifa Rais Magufuli amekuwa akiipatia heshima kubwa nchi ya Tanzania kwa mapambano yasiyokoma dhidi ya rushwa hivyo taasisi za kimataifa ikiwemo TRANSPARENCY INTERNATIONAL zimeonesha Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika miaka hii mitatu ikitoka nafasi ya 117 hadi 99.

Aidha, Dkt. Abbasi ameongeza kuwa, Novemba, 2018 Serikali ya Nigeria ilitoa Tuzo ya Uongozi Bora kwa viongozi mbalimbali duniani akiwemo Rais Magufuli, mara baada ya Maonesho ya Kimataifa ya Sanaa na Ufundi yaliyofanyika nchini humo.

“Jumla ya washiriki 123,446 walipiga kura kwenye tovuti ya Jarida la ALM kutoka Afrika na sehemu mbalimbali duniani, huku wengine 33,000 wakitumia mitandao ya kijamii na 3,400 wakituma maoni yao kupitia baruapepe na majukwaa mengine hivyo ili kupata ushindi huo. Rais Magufuli aliwashinda viongozi wengine mashuhuri wa Afrika ambao ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha APC, Nigeria, Chifu Bola Ahmed Tinubu, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini na Rais Nana Akufo-Addo wa Ghana”ameeleza Dkt. Abbasi.

Akizunguza kuhusu hali ya uchumi nchini Dkt. Abbasi ameeleza kuwa, Serikali inaamini Mwaka huu 2019 ukuaji wa uchumi nchini utafika asilimia 7.2 na kuifanya Tanzania kuendelea kuwa katika mataifa matano Afrika kwa uchumi unaokua kwa kasi na kuendelea kuwemo katika 10 ya dunia.

          “Tanzania imekuwa nchi ya tano barani Afrika katika ukuaji wa uchumi na hii inatokana na utekelezaji wa miradi na huduma mbalimbali za kiuchumi zinazoendelea”  amesema Dkt. Abassi.

Mbali na hayo Dkt. Abbasi amesema kuwa Serikali itaendelea kutekeleza kwa kasi wajibu wake kwa umma ikiwemo kuhakikisha hali ya amani, utulivu, kusimamia utawala bora na utawala wa sheria.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO