Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Taifa Linakwenda Katika Mwelekeo Mzuri-Rais Dkt. Magufuli

Posted on: February 5th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia Watanzania wote kuwa Taifa linakwenda katika mwelekeo mzuri hasa baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha uchumi na huduma za kijamii kama vile afya, elimu, maji, nishati na miundombinu ya usafiri.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 05 Februari, 2019 alipokutana na wananchi katika Mtaa wa Zanaki, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kutembelea kampuni ya Africa Media Group (AMGL) yenye vituo vinne vya televisheni ikiwemo channel Ten na vituo viwili vya redio ikiwemo Magic FM, ambayo kwa sasa inamilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mhe. Rais Magufuli amesema pamoja na mafanikio hayo, Serikali itaendelea kupambana na dhuluma na matumizi mabaya ya rasilimali za Taifa na ametoa wito kwa Watanzania wote kuiunga mkono kwa kuhakikishia wanatanguliza maslahi ya Taifa.

Akiwa ndani ya jengo la AMGL, Mhe. Rais ambaye ni Mwenyekiti CCMamejionea mitambo, chumba cha habari na studio za kurushia matangazo za kituo cha redio cha Magic FM na kituo cha televisheni cha Channel Ten, na pia amezungumza na wafanyakazi ambao wamemueleza changamoto mbalimbali zikiwemo uhaba na uchakavu wa vitendea kazi, maslahi madogo ya wafanyakazi na uchakavu wa jengo la kituo hicho.

Mhe. Rais Magufuliameahidi kutoa shilingi Milioni 200 ndani ya siku 2 kwa ajili ya kununulia vitendea kazi vya kituo hicho na pia amewataka wafanyakazi wa AMGL kumpelekea mapendekezo ya jengo lolote la CCM lenye hadhi nzuri ili kuhamishiwa kituo hicho.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza wafanyakazi hao kwa kazi nzuri wanazozifanya na amesema kuwa dhamira yake ni kuhakikisha kituo hicho kinaboreshwa, matangazo yake yanafika maeneo mengi ya ndani na nje ya nchi na kinakuwa kituo cha mfano kwa vituo vingine hapa nchini.

Pia amewataka wafanyakazi hao kujenga umoja wa dhati, kuchapa kazi kwa juhudi zaidi ili kuongeza uzalishaji wa mapato na kuzalisha maudhui ambayo yatawasaidia Watanzania kupata manufaa kama vile kutoa elimu ya kilimo, biashara, ufugaji na uvuvi.

“Nataka Africa Media Group Ltdiwe na vyombo vyenye nguvu, vinavyotazamwa kila mahali hapa nchini hadi nje ya nchi, Tanzania haiwezi kuwa soko la kuangalia vyombo vya habari vya kutoka nje ya nchi, watu waangalie vyombo vya habari vya nje lakini vyombo vyetu viwe ndio mwongozo wa maisha ya Watanzania zaidi ya Milioni 50.

“Na hii natoa wito kwa vyombo vyote vya Tanzania, mna wajibu wa kuzungumzia mazuri ya Tanzania, lakini pia muendelee kutoa elimu kwa Watanzania, Watanzania karibu asilimia 75 ni wakulima, toeni vipindi vya kuonesha kilimo bora, ufugaji bora, nakadhalika” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Baada ya kutoka AMGL, Mhe. Rais Magufuli amekagua mradi wa ukarabati mkubwa wa jengo la kitega uchumi la CCM(SUKITA) lililopo mtaa wa Lumumba Jijini Dar es Salaam ambalo litakamilika mwezi Juni mwaka huu, na akiwa nje ya jengo hilo amesalimiana na wananchi wakiwemo wafanyabiashara ndogondogo ambao amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutimiza wajibu wake wa kuwapigania Watanzania wote bila kubagua.

Mhe. Rais Magufuli amemalizia ziara yake kwa kutembelea Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba Jijini Dar es Salaam na kuzungumza na wafanyakazi ambapo amewahakikishia kuwa chama chao (ambacho ni chama tawala) kinakwenda vizuri hasa baada ya hatua zilizochukuliwa kusimamia misingi ya chama, mali na mapato ya chama, maadili na uongozi na pia kurejesha mali za chama zilizokuwa mbioni kupotea.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

05 Februari, 2019

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO