Idara ya Habari-MAELEZO
Idara ya Habari-MAELEZO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Idara ya Habari-MAELEZO

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Idara ya Habari
    • Dhima na Dira
  • Utawala
    • Watumishi wa Idara
    • Muundo wa Idara
    • Vitengo
  • Huduma zetu
    • Ukumbi wa Mikutano
    • Taratibu za leseni
    • Kitambulisho cha Mwanahabari
    • Tozo za Huduma
  • Machapisho
    • Sheria
    • Kanuni
    • Fomu
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha za Mnato
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoanza
    • Miradi Ijayo
  • Dawati la Matangazo

Waziri Mkuu ampa siku 15 mweka hazina Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge.

Posted on: August 10th, 2017

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamempa siku 15 Mweka Hazina wa Wilaya ya Sikonge, Bw. Evans Shemdoe ajieleze nikwa nini ameshindwa kufikisha asilimia 80 ya makusanyo ya ndani.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Alhamisi, Agosti 10, 2017 wakati akizungumza na watumishi nawatendaji wa wilaya hiyo, mjini Sikonge wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora..

“Nataka maelezoyakayoniridhisha ni kwa nini hamkufikisha asilimia 80 ya makusanyo yahalmashauri ambacho ni kiwango cha chini. Nzega TC wamefikisha asilimia 112,Kaliua wana asilimia 91, Nzega DC wana asilimia 80, ni kwa nini wewe umeshindwakufikisha kiwango hicho?,” alihoji Waziri Mkuu. 

“Ninataka nipate maelezo piani ipi mipango yenu ya kukusanya mapato kwa maeneo mliyoshindwa kufanya vizuri,na pia mmejipangaje kwa mwaka ujao wa fedha. Niyapate maelezo hayo ifikapotarehe 25 Agosti,” amesema.

Alipopewa nafasi yakujieleza, Bw. Shemdoe alisema wamefikisha asilimia 76.7 na wameshindwa kufikialengo kwa sababu ya upungufu wa mvua katika msimu uliopita, hali ambayoilichangia kushuka kwa mavuno ya zao la tumbaku miongoni mwa wakulima.

Hata hivyo, Waziri Mkuualiwataka watumishi wa wilaya hiyo, washirikiane na watendaji na madiwani ilikuongeza mapato ya wilaya hiyo badala ya kuwaachia watendaji wa kata peke yao.

Mara baada ya kupokea taarifaya mkoa wa Tabora, Waziri Mkuu alizitaka Halmashauri tano kati ya nane za mkoahuo zitoe maelezo ni kwa nini zimeshindwa kufikisha asilimia 80 ya makusanyokama ambavyo waliagizwa na Serikali.

“Halmashauri zilizovukamalengo ni tatu tu, Nzega TC, Kaliua na Nzega DC. Nataka taarifa za halmashaurizilizobakia ifikapo Agosti 25, wakijieleza ni kwa nini hawajafikia malengo yaukusanyaji mapato yaliyowekwa ambayo ni asilimia 80,” alisema.

Taarifa ya mkoa huoinaonyesha makusanyo kwa kila Halmashauri ni kama ifuatavyo:- Tabora Manispaaasilimia 64.1; Nzega Mji (asilimia 112); Nzega Wilaya (asilimia 80.8); Igunga(asilimia 64.6); Tabora (asilimia 77.3); Sikonge (asilimia 76.7); Urambo(asilimia 70.9) na Kaliua (asilimia 91.5).

Pia amezitaka Halmashaurizote zihakikishe zinafanyamakusanyo kwa kutumia mfumo wa kielektroniki.“Ukusanyaji wote wa mapato ni lazima ufanyike kwa mfumo wa kielektroniki.Halmashauri ambazo hazijafanya hivyo, zitumie makusanyo ya mwaka jana kununuliamashine za EFD. Hatutaki kuona risiti za kuandika kwa mkono zinatumika,”alisisitiza.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa mkoa wa Tabora uhakikishe wanapatikanawatumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika wilaya hiyo ili wawezekusaidiana na watendaji wa halmashauri hiyo kukusanya mapato.

“Hapa Sikonge naambiwa hakunaofisi za TRA. Lazima tupate maafisa wa TRA katika kila Halmashauri ili watoeelimu na washirikiane na madiwani, watendaji wa vijiji na watumishi waHalmashauri juu ya ukusanyaji mapato,” alisema.

Matangazo

  • Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari May 03, 2023
  • Baraza la Mawaziri April 14, 2023
  • Uzinduzi wa ‘The Royal Tour’ katika Ukumbi wa Guggenheim uliopo Manhattan, Jijini New York nchini Marekani April 19, 2022
  • Launch of 2019 SADC Media Awards February 13, 2019
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisaini nakala 3 za Sheria za Tanzania zilizofanyiwa urekebu kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha Sheria ya urekebu wa sheria, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 23 Aprili, 2025.

    April 23, 2025
  • The Global Goalkeepers Award

    February 04, 2025
  • Mkutano wa Tatu wa Nchi zinazozalisha Kahawa Barani Afrika

    January 28, 2025
  • Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika kuhusu Masuala Nishati

    January 28, 2025
  • Angalia zote

Wasiliana Nasi

Makole, Uhindini

S.L.P: S.L.P 677, Dodoma

Simu: +255-22-2771005

Nukushi:

Email: maelezo@mawasiliano.go.tz

Simu ya Kiganjani:

Kiunganishi cha Haraka

  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari
  • Kanuni za Sheria za Huduma za Habari za Mwaka 2017
  • Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016
  • Fomu ya Kitambulisho cha Mwanahabari aliyopo nje ya Tanzania
  • Maelezo Podcasts (Apple Podcasts)
  • Maelezo Podcasts (Spotify)
  • Maelezo Podcasts (Amazon Music)
  • Tanzania 'THE ROYAL TOUR'
  • Tanzania 'The Royal Tour' AMAZON
  • HOTUBA YA WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHESHIMIWA NAPE MOSES NNAUYE (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA WA FEDHA 2022/23
  • Baraza la Mawaziri
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIHUTUBIA KATIKA MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA (UN) TAREHE 23 SEPTEMBA, 2021 JIJINI NEW YORK, NCHINI MAREKANI
  • NCHI YETU - MIAKA 61 YA UHURU
  • NCHI YETU - Miaka Miwili na Samia
  • Mjadala maalum kuhusu mpango wa uwekezaji katika Bandari zetu!

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Ofisi ya Rais Zanzibar
  • Tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais
  • Tovuti ya Rais-IKULU
  • Southern African Development Community
  • Tovuti ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Video za Hivi Karibuni

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2023 Habari - MAELEZO